Litania ya Bikira Maria, Rozari Takatifu

LITANIA YA BIKIRA MARIA
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize


Baba wa mbinguni Mungu,
Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu,
Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja
Utuhurumie

Maria Mtakatifu, 

Utuombee

Mzazi Mtakatifu wa Mungu,
Bikira Mtakatifu, Mkuu wa mabikira,
Mama wa Kristu,
Mama wa kanisa, 
Mama wa neema ya Mungu,
Mama mtakatifu sana,
Mama mwenye usafi wa moyo,
Mama usiye na doa,
Mama usiye na dhambi,
Mama mpendelevu,
Mama mstaajabivu,
Mama wa shauri jema,
Mama wa Mwumba,
Mama wa Mkombozi,
Bikira mwenye utaratibu,
Bikira mwenye heshima,
Bikira mwenye sifa,
Bikira mwenye enzi,
Bikira mwenye huruma,
Bikira amini,
Kikao cha haki,
Kikao cha hekima,
Sababu ya furaha yetu,
Chombo cha neema,
Chombo cha heshima,
Chombo bora cha ibada,
Waridi lenye fumbo,
Mnara wa Daudi,
Mnara wa pembe,
Nyumba ya dhahabu,
Sanduku la Agano,
Mlango wa mbingu,
Nyota ya asubuhi,
Afya ya wagonjwa,
Makimbilio ya wakosefu,
Mfariji wa wenye uchungu,
Msaada wa Wakristu,
Malkia wa Malaika,
Malkia wa Mababu,
Malkia wa Manabii,
Malkia wa Mitume,
Malkia wa Mashaidi,
Malkia wa Waungama,
Malkia wa Mabikira,
Malkia wa Watakatifu wote,
Malkia uliyeumbwa, pasipo dhambi ya asili,
Malkia uliyepalizwa mbinguni,
Malkia wa Rozari takatifu,
Malkia wa amani.


Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia
Utusamehe Ee Bwana

Mwanakondoo wa Mungu uondoae dhambi za dunia
Utuhurumie Ee Bwana

Mwanakondoo wa Mungu uondoae dhambi za dunia
Utuhurumie Ee Bwana

K. Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu.
W. Tujaliwe ahadi za Kristu.

TUOMBE:
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako tuwe siku zote na afya ya roho na ya mwili. kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakatifu, Bikra daima, tuopolewe na mashaka ya sasa, tupate furaha za milele. Kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina. 


KUMBUKA
Kumbuka, ee Bikira Maria mwenye rehema, haijasikilika kamwe kwamba ulimwacha mtu aliyekimbilia ulinzi wako, akiomba shime kwako, akitaka umwombee. Nami kwa matumaini hayo, nakukimbilia, ee Mama, mkuu wa mabikira; ninakuja kwako, nasimama mbele yako nikilalamika mimi mkosefu, ewe Mama wa Neno wa Mungu, usiyakatae maneno yangu, bali uyasikilize kwa wema, na unitimizie. Amina.


SALAMU MALKIA
Salamu, Malkia, Mama mwenye huruma; uzima, tulizo na matumaini yetu, salamu. Tunakusihi ugenini hapa sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi, Mwombezi wetu, utuangalie kwa macho yako yenye huruma. Na mwisho wa ugeni huu, utuonyeshe Yesu, mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, ee mwema, ee mpendevu, Bikira Maria.

K. Utuombee, Mzazi mtakatifu wa Mungu. 
W. Tujaliwe ahadi za Kristu.

Tuombe: 
Ee Mungu, makimbilio na nguvu yetu, uwaangalie kwa wema watu wanaokulilia; na kwa maombezi ya Bikira Maria mtukufu asiye na kosa, Mzazi wa Mungu, na ya Mtakatifu Yosefu, mchumba wake, na ya Watakatifu Petro na Paulo Mitume wako, na ya Watakatifu wote: usikilize kwa huruma na wema sala tunazokutolea kwa wongofu wa wakosefu na kwa uhuru na utukufu wa Kanisa, mama mtakatifu. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.

Asanteni kwa kuwa nasi. Mtangulize Mungu kwa kila jambo lako. Hapa chini ni sala muhimu, bonyeza tu. 
πŸ’  SALA YA ASUBUHI
πŸ’  SALA YA USIKU
πŸ”ΉπŸ”ΉπŸ”Ή
Usisite kutuandikia hapo chini (Enter Comment) maoni yako, umejifunza nini, umefurahishwa na kipi au una mapendekezo gani kwa #visiontanzania.....
πŸ”ΉπŸ”ΉπŸ”Ή

♂️MENU


Comments

Popular Visiontanzania Posts

KIJANA MIAKA 18-35 USIKOSE HII

ACADEMY MEMBERSHIP ONLINE APPLICATION For VISION ENTREPRENEURSHIP ACADEMY

MENU

NGUZO KUU 8 ZA MAFANIKO KATIKA JAMBO LOLOTE

MFAHAMU FLAVIANA MATATA MPAMBANAJI TOP

HISTORIA YA SAID SALM BAKHRESA

MAMBO YALETAYO FURAHA YA KWELI MAISHANI

FUNZO KUU LA KUFANIKIWA ATOA JACK MA

NJIA RAHISI YA KUISHI NDOTO ZAKO